MAHITAJI NA VIPIMO.
i. Boga - 1
ii. Tui La Nazi - 2 Vikombe
iii. Sukari - 1 kikombe
iv. Hiliki - 1/2 kijiko cha chai
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Unamenya maboga kiasi ukipendacho.
2. Unayakata kata vipande vidogo vidogo.
3. Unayachemsha mpaka yawive lakini humwagi maji wala yasije kuvurugika.
4. Maji yakishaanza kukauka unatia sukari kiasi ukipendacho na hiliki.
5. Kisha unamimina tui la nazi.
6. Unaiwacha ichemkie na kabla kukauka tui unaepuwa na tayari kuliwa.

No comments:
Post a Comment